Musa Mwarabu

Musa Mwarabu aliishi miaka mingi ya karne ya 4 kama mkaapweke maarufu kati ya Misri na Syria,[1] kabla hajafanywa askofu wa kwanza wa Kiarabu kati ya Waarabu kutokana na sharti la malkia wao, Mavia, kwa ajili ya kusimamisha mapigano yake na Dola la Roma.[2]

Kama askofu Musa hakuwa na makao maalumu, bali alifuata tabia ya uhamaji wa watu wake, akiwaongoa wengi na kudumisha amani kati yao, tena kati yao na dola hilo.[1]

Alifariki mwaka 389 hivi.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 7 Februari[3][4].

  1. 1.0 1.1 Butler and Burns, 2000, p. 68.
  2. Jensen, 1996, pp. 73-75.
  3. Martyrologium Romanum
  4. Bunson et al., 2003, p. 595.

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search